Tuesday, February 3, 2015

MRADI WA MAJI WA MASOKO WAZIDI KUUMIZA VICHWA VYA MADIWANI WIRAYANI RUNGWE KUTOKANA NA WANANCHI WA KATA YA MASOKO KUSUSIA KUPIGA KURA YA MAONI YA KATIBA MPYA NA UCHAGUZI MKUU BAADA YA MRADI WA MAJI WA MASOKO KUTO KAMILIKA TANGU MWAKA 2012 HADI SASA WANANCHI WANAKOSA MAJI

SEHEMU YA MADIWANI WA BARAZA LA HALMASHAURI YA RUNGWE

SEHEMU YA WATENDAJI WA HALMASHAURI YA RUNGWE


MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA RUNGWE MHE MWAKASANGULA DIWANI WA KATA YA KISONDELA AKIONGOZA KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI WA HALMASHAURI YA RUNGWE KIKAO KILICHOKUWA NA AJENDA SITA LAKINI KATIKA MUDA WA MASWALI NA MAJIBU NDIPO KULIJITOKEZA NA SWALI LINALOHUSU MRADI WA MASOKO AMBAO UMEKUWA KAMA AJENDA YA KUDUMU KATIKA VIKAO VYA BARAZA LA RUNGWE  HUKU TANGU MWAKA 2012 WANANCHI WA KATA YA MASOKO WANAKOSA MAJIWALIYO TARAJIWA KUYAPATA

BAADA YA KUULIZWA SWALI LA MSINGI KUHUSU MRADI WA MASOKO NA KUTOTEKELEZWA Mhe. Rephson Mwaisupule DIWANI WA KATA YA MASUKURU AMESEMA KUWA MAJIBU SIJARIDHIKA NAYO KWAKUWA MRADI WA MASOKO UNAITIA DOA HALMASHAURI NA SASA HALMASHAURI ITAFILISIWA MALI ZAKE KWA KUWA HADI SASA INADAIWA TSH 786,426,316.70/= AMBAZO NI PESA HARALI AMBAZO MKANDARASI ANATAKIWA KULIPWA KULINGANA NA KAZI ALIZOZIFANYA KATIKA MRADI WA MASOKO


WATENDAJI WA HALMASHAURI YA RUNGWE WAKIWA MAKINI KUSIKILIZA MAELEZO YANAYOTOLEWA NA MADIWANI KUHUSU HUJUMA ZINAZOFANYIKA KATIKA MRADI WA MASOKO WILAYANI RUNGWE

AKIONGEA KWA HISIA KALI NA KWA MASIKITIKO YA WANACHI WALIOTARAJIA KUPATA MAJI HADI SASA HAWAJAPATA MAJI HATA TONE MHE, EZEKEA MWALUSAMBA DIWANI WA KATA YA BAGAMOYO AMESEMA KUWA MCHEZO UNAOENDELEA HUU MCHAFU WA KUWAZURUMU WANACHI WASIPATE MAJI UNA WATU WENGI SANA WANAOIHUJUMU HALMASHAURI YA RUNGWE KWA KUJINUFAISHA WENYEWE, NA AMEOMBA UCHUNGUZI UANZIE KWA MADIWANI NA WATENDAJI WALIOHUSIKA PIA WANASIASA WALIONYUMA KUUHUJUMU MRADI WA MASOKO WACHUNGUZWE NA WOTE WACHUKULIWE HATUA ZA KISHERIA

DIWANI WA KAMBI YA UPINZANI MHE, MWASAKILALI WA CHAMA CHA NCCR AMESEMA KUWA KUTOTEKELEZWA KWA MRADI WA MASOKO NI PIGO KUBWA NA NI ANGUKO LA CCM KATIKA UCHAGUSI MKUU WA MWAKA HUU KWAKUWA WANANCHI WANAHITAJI MAJI LAKINI WATENDAJI WACHACHE NA WANASIASA WANAFANYA MRADI USITEKELEZWE KWA MANUFAA YAO BINAFSI


AKITOA USHAURI MBELE YA BARAZA LA MADIWANI MHE, RAULENTH KWAKALIBULE DIWANI WA KATA YA  KIWIRA KUPITIA CHADEMA AMESEMA KUWA KUWA MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA RUNGWE UMEPEWA DHAMANI YA KUONGOZA NA KUSIMAMIA YALE YOTE YANAYOPITISHWA NA BARAZA NA SIO VINGINEVYO HIVYO KUYUMBISHWA KWA MAAMUZI YANAYOTOLEWA NA MADIWANI NI KUTOSIMAMIA IPASAVYO NA KUTOJITAMBUA KAMA VIONGOZI MLIOPEWA DHAMANA YA KUONGOZA HALMASHAURI KWA UAMINIFU

MHE, MADODI WA KATA YA BAGAMOYO AMESEMA KUWA WASIWASI NI KUWA UTENDAJI WA OFISI YA HALMASHAURI YA RUNGWE IMEWEZEJE KUPOTEZA NYARAKA MUHIMU AMBAZO ZIMEFANYA HALMASHAURI KUKOSA NYARAKA ZINAZOPELEKEA HALMASHAURI KUSHINDWA KESI NA KUFIKIA HATUA YA KUFILISIWA?

AKIONGEA KWA UNYENYEKEVU MWENYEKITI WA KAMATI YA MAJI YA HALMASHAURI YA RUNGWE AMESEMA KUWA PAMOJA NA KUTUMWA NA BARAZA LA MADIWANI KWENDA DODOMA TAMISEMI NA OFISI YA WAZIRI MKUU AKIWA NA MWENYEKITI WA HALMASHAURI KUSHUGHURIKIA SUALA HILI LA MARADI WA MASOKO YEYE KAMA MWENYEKITI WA KAMATI YA MAJI ANASHANGAA KUWA TAARIFA WANAZOZILETA KUTOKA TAMISEMI NA OFISI YA WAZIRI MKUU  WAZILETWI KATIKA VIKAO HUSIKA ILI ZIJADILIWE KWA MANUFAA YA WANANCHI WA MASOKO NA RUNGWE. HIVYO AMEWATAKA MADIWANI KUMSAIDIA MWENYEKITI KWAKUWA AMEZIDIWA NA WATU WACHACHE WASIYOITAKIA MEMA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUNGWE NA AMEWATAKA MADIWANI KUIJADIRI HOJA HII UPYA KWA MASLAHI MAPANA YA WANANCHI WA RUNGWE

AKITOA USHAURI KWA MADIWANI WA MADIWANI KUPEWA SEMINA KUHUSU SUALA LA MASOKO MKUU WA WILAYA YA RUNGWE CHRISPIN MEELA AMESEMA KUWA SIKU IPANGWE ILI MADIWANI WAPATE SEMINA YA KUUJUA MRADI WA MASOKO NA NINI KINAENDELEA NA KUPELEKEA WANANCHI WA MASOKO KUKOSA MAJI TANGU MWAKA 2012 HADI SASA

AKIMSHUKURU MWENYEKITI  KWA KUTENGUA KANUNI NA KUSABABISHA MADIWANI KUJADILI KWA KINA NA AMESEMA KUWA UTENDAJI MBOVU NA PIA KUWA KUNA MADIWANI WANAFKI SANA AMBAO WANAJIPENDEKEZA KWA MKUU WA WILAYA NA MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA RUNGWE ILI TU MRADI HUU WA MASOKO KUTOFANIKIWA HADI SASA.

AJENDA YA MRADI WA MASOKO ILIFUNGWA KWA KUHITIMISHA KUWA MWEZI WA TATU KIKAO MAALUM KITAKAA KUTENGUA MAAZIMIO YA KUKATA RUFAA NA KUFUATA USHAURI WA TAMISEMI NA OFISI YA WAZIRI MKUU PIA USHAURI ULIOTOLEWA MBELE YA BARAZA LA MADIWANI KUPITIA MWANASHERIA WAKE MERICK LUVINGA KUWA ILI HALMASHAURI KUENDELEA NA MRADI WA MASOKO INATAKIWA MKANDALASI ALIPWE KWANZA MADAI YAKE YOTE KWAKUWA NI STAHIKI YAKE
 
Mradi wa maji wa masoko umeendelea kuumiza vichwa vya madiwani na watendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Rungwe baada ya kesi ya jinai ya kughushi nyaraka za bondi kuonekana kuwa na changamoto kubwa  kutokana  Halmashauri ya wilaya ya Rungwe kukosa nyaraka harisi za dhamana za mradi wa maji wa masoko hivyo kupelekea halmashauri ya wilaya ya Rungwe kusababisha kuchelewa kukamilika kwa mradi kwa sababu ya kuendesha kesi isiyokuwa na ushahidi huku wananchi wa Masoko wakiendelea kukosa maji .

Akitoa majibu ya maswali ya juu ya mradi wa maji masoko yaliyoulizwa na diwani wa kata masukulu Mhe. Rephson Mwaisupule yaliyo ulizwa  juu ya hatua za rufaa ya kesi ya awali kushindwa na kutakiwa kulipa  Tsh 786,426,316.70 pia hatima ya kesi ya jinai ya kughushi nyaraka za bondi  na kuagiza ofisi ya mkurugenzi  itafute nyaraka husika na kuziwasilisha polisi.

Mkurugezi wa wilaya ya Rungwe Mhe.bi Veronica Kessy amesema kwamba  suala la kesi ya kughushi nyaraka ufuatiliaji unaendelea kufanyika katika taasisi mbalimbali ikiwemo TAKUKURU, BANK na kwa wahusika ambako nyaraka hizo zilipita mikononi mwao.
Ofisi ya mkuu wa upererezi imesema kwamba “shauli la jinai hilo liko katika hatua za mwisho za kiupelelezi na kinachokwamisha  ukamilishaji wake ni ofisi yako (ya mkurugenzi wa halmashauri ya wiraya ya Rungwe) kushindwa kuwasilisha  katika ofisi hii nyaraka halisi ambazo ni Perfomance Bank Guarantee no.611512/L.32/201 ya tarehe 20.7.2010,Extension of perfamance Bond ya tarehe23.11.2011 na Extension of performance Bank Guarantee ya tarehe 20.7.2010, nyaraka ambazo zinatakiwa kwa ajili ya kuzipereka katika maabara ya uchunguzi wa kisayansi(FB) Dar es salaam pamoja na sampuli za saini na sampuli za muhuri wa moto ili zifanyiwe uchunguzi wa kitaalam”.

Ufuatiliaji uliofanywa na Bank ya NBC makao makuu Dar es salaam wamerudisha majibu kuwa nyaraka hizo hazipo chini ya Bank na nyaraka halisi huwa zinabaki kwa mnufaika. Hivyo Halmashauri ya wilaya ya Rungwe imeamua  kuendelea kutafuta nyaraka hizo  kwa kumuandikia barua Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Iramba  ambako John  Shirima amehamishiwa na kufanya kazi huko ambaye alikuwa ndiye mhasibu na mtunzaji wa nyaraka hizo,kupitia Mkurugenzi wake aweze kuja kukabithi nyaraka hizo hazipo katika taarifa yake ya kukabidhi ofisi.

Nao madiwani wakiongozwa na diwani wa kata ya masukulu aliye pinga majibu ya Mkurugenzi, na kusababisha mjadala mzito ndani ya kikao hicho na kumshambulia Mkurugenzi kuwa kuna mtu anafanya kazi  kwa kumuendesha  Mkurugezi  na mwenywkiti nje ya vikao halali vya madiwani na kuwa Mkurugezi ataadhimiwa na baraza na kuondoka na huyo mtu.

Wakiongea kwa hisia kali na kuonekana kukerwa na utekelezaji mbovu wa mradi  wa masoko ambao umekuwa kelo kwa wananchi kwa mda mrefu, diwani wa kata ya Bulyaga mesema kwamba Halmashauri haina vielelezo  au nyaraka hizo na wamemtaka Shirima ashitakiwe kwa kuhusika kupoteza nyaraka makusudi na kusema kuwa kuna  kundi lililofanya ubadhilifu huo ni kubwa na wananchi wa masoko hawahitaji propaganda za kisiasa na kujinufaisha wenyewe zaidi ya wananchi  kupata maji wanayoyasubili kwa mda mrefu bila mafanikio.

Baada ya Sakata la kukata rufaa kushindikana kabisa baraza rimerejea ushauri wa mwana sheria wa Halmashauri ya wilaya ya Rungwe  Merick Luvinga ambapo kikao cha awali aliishauri baraza kuwa kutokana na Halmashauri kutokuwa na nyaraka,hawawezi kushinda kesi mahakamani hivyo aliitaka Halmashauri imlipe mkandarasi na kufuata  ushauri uliotolewa na tamisemi waliounda kamati ya watu watano akiwemo mwanasheria na mkaguzi wa ndani wa tamisemi baada ya kuona kuwa pande zote zinamakosa na kushauri mkandarasi wa kwanza aendelee na shughuri hiyo ili halmashauri isije kufilisiwa na mkandalas kutokana  na pesa anazodai mkandalasi.Tsh.mil 786,426,316.70.

Kufuatia na kuendelea kwa mgogoro huu wa utekerezaji mbovu wa mradi wa maji wa masoko, wananchi hao kwa pamoja  walipotembelewa na kamati ya kudumu ya maji kilimo na mifugo iliyokuwa imeongozwa na  Mhe. Prf Peter Kusolwa wananchi hao walieleza kuwa hawapo tayari kushiriki kupig kura ya katiba ya maoni na uchaguzi mkuu mwaka huu kwa kuwa ni serikari haijamilisha mradi wa maji tangu mwaka 2012 hadi sasa wananchi wanakosa maji kwa sababu za watu wachache wasio waaminifu.

TUMAIN OBEL

KINGOTANZANIA - 0752 881456

No comments: