Wednesday, February 4, 2015

WANASHERIA NCHINI CHANZO CHA MIKATABA MIBOVU ;CHRISIPIN MEELA

MGENI RASMI MKUU WA WILAYA YA RUNGWE CHRISPIN MEELA AKIONGEA NA WANANCHI WALIOJITOKEZA KATIKA MAADHIMISHO YA SHERIA NCHINI, AMEWATAKA WANASHERIA KUTUMIA VIZURI TAALUMA WALIYONAYO

HAKIMU MKAZI MFAWIDHI WILAYA YA RUNGWE OMARI KINGWELE AKIJIBU MASWALI YALIYO ULIZWA NA WANANCHI WALIOHUDHURIA MAADHIMISHO YA SIKU YA SHERIA NCHINI AMBAPO AMESEMA ILI HAKI IWA NA MAANA NI RAZIMA IPATIKANE KWA HAKI NA KWA MUDA MUAFAKA

WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUNGWE NA WAGENI WAARIKWA WAKISIKILIZA NYIMBO KUTOKA KWA WANAFUNZI WA SHULE YA SEKONDARI YA BUJINGA

MEZA KUU IKITAZAMA IGIZO KUTOKA KWA WANAFUNZI WA SHURE YA SEKONDARI YA BUJINGA KUTOKA KUSHOTO NI MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUNGWE MHE.MWAKASANGULA,HAKIMU  MKAZI MFAWIDHI WA WILAYA YA RUNGWE MHE.OMARI KINGWELE,MKUU WA WILAYA YA RUNGWE CHRISPINI MEELA NA MWAKILISHI WA CHAMA CHA SHERIA TANGANYIKA MHE. A.MBOGO
WAGENI WAARAKWA WAKISIKILIZA HOTUBA KUTOKA KWA MGENI RASMI



WANAFUNZI WA SHURE YASEKONDARI YA BUJINGA WAKITOA BURUDANI YA MAIGIZO YENYE UJUMBE WA RUSHWA MAHARA PA KAZI
BAADHI YA WATUMISHI WA MAHAKAMA WAKISIKILIZA HOTUBA KWA MAKINI



PICHA YA PAMOJA YA WATUMISHI WA MAHAKAMA NA WAKUU WA TAASISI MBALIMBALI WILAYANI RUNGWE



Wanasheria wamekuwa chanzo cha majanga na mikataba mibovu hapa nchini kwani wao ndio wanasababisha Taifa kuingia katika mikataba mibovu,ufisadi na chanzo cha kupoteza watumishi  wa umma wenye utendaji mzuri wa kazi.

 Chrispin Meela Mkuu wa wilaya ya Rungwe akiongea na wananchi wa wilaya ya Rungwe waliojitokeza katika viwanja vya mahakama ya wilaya ya Rungwe katika siku ya sheria nchini, yaliyofanyika katika viwanja vya  mahakama ya Hakimu mkazi wa wilaya ya Rungwe, yenye kauli mbiu ‘‘FURSA YA KUPATA HAKI: WAJIBU WA SERIKALI, MAHAKAMA NA WADAU’

 Mkuu wa wilaya ya Mhe. Chrispin Meela amesema kuwa watumishi wengi  wa wanasheria Tanzania waliopewa dhamana ya kuandaa mikataba mablimbali na kusaini,hivyo kupelekea mikataba mibovu iliyo  kuwanasaini na isiyokuwa na tija kwa taifa na kufanya vitu vya manufaa yao wenyewe  sio kwa Tanzania.

Pia Chrispini Meela amewataka wanasheria kutumia taaluma yao vizuri na  kwani wao ndio wanasababisha wananchi kuchukia serikali na chama tawala kutokana na mikataba mibovu wanayoishauri serikali na kupoteza watumishi wazuri kwa ushauri wanaotoa.hata hivyo ameitaka mahakama  kuwa kesi zisizomaliza upelelezi kwa mda mrefu na kwa uzembe zifutwe na atakee chelewesha kesi kwa makusudi kwa kutoleta mashahidi mahakama wawe wakali na wamchukulie sheria  kwani kuchelewesha kesi kunasababisha mahakama ichukiwe na wananchi na ameomba mahakama za mwanzo kupunguza mashariti ya dhamana kulingana na kesi yenyewe. 

Akimkaribisha mgeni rasmi Hakimu Mkazi Mfawidhi wa wilaya ya Rungwe Mhe. Omari Kingwele amesema ili haki iwe na maana ni razima ipatikane kwa haki na kwa muda muafaka lakini kesi nyingi huchelewa pale mmoja wapo anaposhindwa kutoa ushirikiano  na kuwa jeshi la polisi ndio wadau wakubwa wa mahakama kwani wao ndio wanaomkamata mharifu na kujua ni aina gani ya ushahidi unaotakiwa  mahakamani.

  Mhe. Kingwele amesema washitakiwa wanaoachiwa huru ni kutokana na kushindwa kupata vielelezo sahihi kutoka kwa wapelelezi na ushirikiano hafifu wa wananchi ndio unapelekea kuachiwa huru hivyo amewataka wananchi kutoa ushirikiano kwani wao ndio chanzo cha awali kufanikisha wajibu wa haki, na kushirikiana na jeshi la polisi kikamilifu ili kufanya kazi kwa uzuri zaidi.

Maadhimisho haya ya Sheria Wilayani Rungwe yamefanyika yakiambatana na burudani za nyimbo na  maigizo kutoka shule ya Sekondari Bujinga Tukuyu mjini, yenye ujumbe wenye maudhui ya Rushwa mahara pa kazi na wananchi walipata fursa ya kuuliza maswali kwa Taasisi zilizokuwepo za  Mahakama, Jeshi la Polisi, Magereza  pamoja na PCCB,na mwisho wananchi walijionea mahakama navyoendesha kesi  na kujifunza  mahakama inavyofanya kazi zake za kila siku.

TUMAIN OBEL
KINGOTANZANIA

No comments: