Watangazaji
wa Azam TV (kutoka kushoto) ni Raymond Nyamwihula, Zainab Chondo,
Rehema Salum, Nurdin Suleiman, Fatuma Almasi Nyangasa, Baruani Muhuza,
Ivona Kamuntu na Charles Hilary.
Kituo cha
Televisheni cha Azam kimefanya mabadiliko katika utangazaji wa taarifa
za habari, huku kikimuajiri Jane Shirima kuwa mkurugenzi wa televisheni.
Kuanzia leo taarifa ya habari ya Azam TV itakuwa ikisomwa na watangazaji wawili na kutakuwa na pea tatu tofauti za watangazaji.
Naibu
Mtendaji Mkuu wa Azam Televisheni, Tido Mhando alisema jijini Dar es
Salaam jana kuwa wamejiandaa vilivyo kuhakikisha kuwa mbali na studio
bora wanakuwa pia na kikosi cha wanahabari wenye uwezo mkubwa.
“Hapana
shaka tunao vijana wazuri sana, lakini pia tulihitaji waandishi wenye
uwezo na ujuzi wa hali ya juu ili kuendana na mikakati, fikara na
mipango yetu ya kufanya mageuzi makubwa ya hali ya utangazaji wa habari
za televisheni nchini,” alisema Tido.
“Duniani
pote vituo vingi vya televisheni na redio vilianzishwa kwa mtindo kama
huu. Kituo cha lugha ya Kiingereza cha Al Jazeera kilipoanzishwa
kiliajiri watangazaji waliobobea kutoka mashirika kadhaa makubwa ya
utangazaji duniani ikiwa ni pamoja na CNN, BBC na NBC. Lakini pia lazima
kuwepo na hadhi ya kuweza kuwavutia watu hao,” alisema mkurugenzi huyo
wa zamani wa redio Idhaa ya Kiswahili ya BBC.
Tido
aliwataja baadhi ya waandishi na watangazaji ambao wameungana na Azam TV
kuwa ni Charles Hilary, Baruani Muhuza, Ivona Kamuntu na Fatuma Almasi
Nyangasa.
“Watangazaji
hao sasa wataungana na wasomaji wetu wazuri wa siku nyingi Rehema Salum
na Nurdin Suleiman kukamilisha pea tatu za wasomaji wa mtindo wa wawili
wawili,” alifafanua Tido.
Tido
alisema leo na kesho habari itasomwa na Charles Hillary na Ivona Kamuntu
wakati siku mbili nyingine itakuwa ni zamu ya Baruhani Muhuza na Fatuma
Nyangasa huku Rehema Salum na Nurdin Suleiman nao wakiwa na zamu yao.
Alisema
licha ya taarifa ya habari ya saa mbili usiku pia wanatarajia hivi
karibuni kuanzisha taarifa ya habari ya saa saba mchana itakayokuwa
ikiendeshwa na Zainab Chondo na Raymond Nyamwihula.
“Mpango
wote huu wa mabadiliko haya ya utangazaji na upatikanaji wa habari wa
Azam TV utakuwa unasimamiwa na kuratibiwa na Joseph Warungu aliyekuwa
Mwafrika wa kwanza kuongoza kitengo cha BBC cha Focus on Africa,”
alisema Tido.
Tido
aliwataja wanahabari wengine mbao wamejiunga na Azam TV kuwa ni Taji
Liundi, Phillip Cyprian, Mwanga Kirahi na Jane Shirima ambaye ataanza
kazi leo kama mkurugenzi wa televisheni.
Wakati
huohuo, Tido alisema kuanzia Jumamosi wiki hii watazindua kipindi
maalumu cha mahojiano ya kina kwa wote waliotangaza na kuchukua fomu za
kugombea nafasi ya urais. Kipindi hicho kinachojulikana kwa jina la
Funguka kitakuwa kinatangazwa kila siku kuanzia saa moja kamili usiku.
Tido alisema katika muda wa mwezi mmoja ujao Radio ya Azam Media Group itakayojulikana kwa jina la UFM itakuwa hewani.
Chanzo:Mwananchi
No comments:
Post a Comment