Wednesday, May 31, 2017

Mbunge wa zamani wa moshi mjini afariki dunia

Dodoma. Mbunge wa zamani wa Moshi Mjini (Chadema) Philemon Ndesamburo amefariki dunia ghafla leo, wakati akipata matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC, Moshi.

Katibu wa Chadema, Mkoa wa Kilimanjaro, Basil Lema amethibitisha kifo hicho na kueleza kuwa wataendelea kutoa taarifa zaidi juu ya kifo cha mwanasiasa huyo mkongwe.

 Taarifa zaidi kuhusu kifo cha Ndesamburo zitaendelea kukujia.

No comments: