Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Mbeya Naibu Kamishina wa Polisi MOHAMMED R. MPINGA ametoa
wito kwa jamii kuondokana na tamaa ya kutaka utajiri kwa njia zisizo halali kwa
kujihusisha na uhalifu na badala yake watafute shughuli halali kwa ajili ya
kujipatia kipato.
Kamanda
mpinga ametoa onyo hilo alipokua akitoa taarifa kwa vyombo vya habari ambapo
ameeleza kuwa Mnamo tarehe 03 Februari, 2018 majira ya saa 12:00 Mchana huko
maeneo ya mtaa wa Mponja – Uyole, Kata ya Igawilo, Tarafa ya Iyunga, Jiji na
Mkoa wa Mbeya, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya kwa kushirikiana na Viongozi wa
Hospitali ya Mkoa wa Mbeya walifanikiwa kumkamata mtu mmoja aliyefahamika kwa
jina la HAPPY CHARLES [24] Mama Lishe, Mkazi wa Airport ya Zamani akiwa na
mtoto mchanga jinsia ya kike aliyemuiba katika Hospitali ya Mkoa wa Mbeya.
Awali mnamo tarehe 01 Februari,
2018 majira ya saa 04:00 usiku huko katika wodi ya watoto Hospitali ya Mkoa wa
Mbeya iliyopo Kata ya Forest Mpya, Tarafa ya Iyunga, Jijini Mbeya, mwanamke
mmoja anayefahamika kwa jina la SARAH MWASANGA [35] Mkazi wa Iganzo akiwa
katika wodi ya wazazi Hospitalini hapo baada ya kujifungua mtoto wa kike
aligundua kuibiwa kwa mtoto huyo na mtu asiyefahamika.
Kutokana na tukio hilo, uongozi
wa Hospitali hiyo ulitoa taarifa kituo kikuu cha Polisi [Central] na ndipo
upelelezi kuhusiana na tukio hilo ulianza kufanyika.
Taarifa
za siri zilipatikana na kubainisha kuwa huko maeneo ya Airport ya zamani kuna
mama mmoja aitwaye HAPPY CHARLES [24] Mkazi wa Airport ambaye hapo awali
alikuwa akimdanganya mume wake aitwaye CHILUBA PETER, Dereva Taxi Hospitali ya
Rufaa Mbeya na Mkazi wa Airport kuwa ni mjamzito na kwamba amejifungua mtoto wa
kike tarehe 31 Februari, 2018 na ndipo ufuatiliaji wa kuwapata watu hao
ulianza.
No comments:
Post a Comment