Katibu
Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia
wananchi wa mjini Singida wakati alipowahutubia katika mkutano wa
hadhara uliofanyika kwenye uwanja vya Peoples mjini humo ambapo mawaziri
mbalimbali wamehudhuria na kuwaelezea wananchi mpiango ya serikali
katika kutekeleza ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 katika mipango
ya maendeleo, Mkutano huu ulikuwa ni wa mwisho kabla ya kumalizia ziara
yake katika mkoa wa Singida hapo kesho kabla ya kuendelea na ziara hiyo
katika mkoa wa Manyara keshokutwa , Ambapo katika ziara hiyo Kinana
anaongozana na Katibu wa NEC Siasa, Itikadi na Uenezi Ndugu Nape Nnauye,
Mawaziri waliohudhuria katika mkutano huo mkubwa ambao umerushwa moja
kwa moja na kituo cha televisheni cha Star Tv ni Dr. Charles Tizeba
naibu waziri wa uchukuzi, Amos makala Naibu Waziri wa Maji, Mwigulu
Nchemba naibu waziri wa Fedha na Uchumi na, Mbunge wa jimbo la Iramba
Mashariki na Naibu Katibu Mkuu wa CCM,Stephen Wasira Waziri
wa Nchi Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu) na Adam Malima Naibu
waziri wa Fedha na Uchumi na viongozi mbalimbali wa kitaifa na mkoa wa
Singida.
Mwigulu
Nchemba naibu waziri wa Fedha na Uchumi na, Mbunge wa jimbo la Iramba
Mashariki na Naibu Katibu Mkuu wa CCM akiwahutubia wananchi katika
mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Peoples mjini Singida
leo.
Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa, Itikadi na Uenezi akiwahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara mjini Singida
Aliyekuwa
mwenyekiti wa CHADEMA jimbo la Singida Mashariki Bw. Andrew Andalu
akipongezwa na Mh. Stephen Wasira mara baada ya alipotangaza kukihama
chama cha CHADEMA na kujiunga na CCM katika mkutano wa hadhara mjini
Singida, kutoka kulia ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Singida Mgana
Msindai, Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana, Mwenyekiti wa CCM
Wilaya ya Singida mjini Khamis Nguli na Mwigulu Nchemba Naibu Katibu
Mkuu wa CCM.












